Mwajiri yeyote anawajibika kuwaandikisha wafanyakazi wake wote alionao na kupewa namba za uanachama ambazo ni lazima kwa mwanachama kuitunza namba hiyo. Mwanachama anawajibika kupewa kitambulisho cha uanachama NSSF/R4 ambacho kinatumia kwa ajili ya kupata mafao na huduma yoyote nyingine kutoka katika Shirika.
Mtu yeyote aliyejiajiri, mkulima, mfanyakazi wa ndani, wafanya biashara wadogo wadogo wanaweza kujiandikisha kwa hiari na kulipia kadiri ya uwezo wao kuanzia shilingi 20,000 kwa mwezi (asilimia 20 ya mshahara wa kima cha chini (KCC) wa serikali) na atapata mafao yote saba yatolewayo na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii.