News
WADAU NA WAKULIMA WA ZAO LA PARACHICHI WANGING'OMBE WAPATA ELIMU YA UMUHIMU WA HIFADHI YA JAMII KUTOKA NSSF
Wafanyakazi wa NSSF wakiongozwa na Meneja wa NSSF Mkoa wa Njombe, Juma Mwita wakitoa elimu kwa Wakulima na Wadau wa zao la Parachichi kuhusu umuhimu wa Hifadhi ya Jamii. Elimu iliambatana na umuhimu wa kujiunga na kuchangia NSSF kupitia Mpango wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi. Mkutano huo wa Wakulima na wadau wa zao la Parachichi uliandaliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe uliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.